NIAZIME KONDOMU, NIPO BAGAMOYO
Hakika
nakuomba msomaji wangu, watu wangu NIAZIMENI KONDOMU usifanye mchezo
nimezidiwa kiasi ambacho inanilazimu kuomba msaada wa kondomu. Haya ni
maisha ya huku sasa, maana kila mmoja anafanya kile anavyojisikia,
ingawaje ni kawaida sana.
Sasa mimi nasema naomba msaada wa kondomu maana usiku nilivyoupitisha, nimeletewa MAKAHABA wawili, halafu kahaba wa pili akaomba kondomu ili amsadie kahaba mwenzie kwakuwa dume lake halikuwa na kondomu.
Siku zote naamini utafiti wakati mwingine inabidi uingie mwenyewe ushuhudie, na mchakato wangu wa kitabu kile ni lazima niingie maeneo magumu yenye vishawishi adhimu. BASI jana usiku nilikuwa na rafiki zangu, na kwakuwa hawa jamaa wamekuja na Wapennzi wao, wakaanza kunishambulia eti nitajiuuuuu(ulikuwa utani) wakati tukiendelea na porojo akaja mzee wa mapokezi akaniambia 'mjukuu usipate taabu wewe sema tu sasa hivi utapata, huu ni mji wa kimataifa bwana'.
Ikabidi nitulie kisha nikamjibu hebu niletee binti mmoja nimchungulie kidogo. Wakati nipo sehemu ya chakula, chumba changu nimekifunga, kumbe yule mzee akampigia simu kahaba mmoja hivi, nadhani anafahamiana nao. Akajiingiza hapa kwenye nyumba tuliyopo, lakini mlango wangu ukawa umefungwa(sikuwepo).
Punde niliporejea, nikaona mzee ananilaumu mbona binti alikuja, ila ameahidi kuwa atakuja tena. Kweli zilipita dakika 15 hivi, nikiwa chumbani naongea na rafiki zangu, mara mlango ukagongwa na yule mzee, nikawaambia jamani waungwana nendeni chumbani kwenu. Mzee akanikabidhi binti tuelewane......
Akakaa kitini na kuniambia anisikiliza, ikabidi niulize inakuwaje mbona unanijia? Akaniambia kuwa alielezwa na mzee kuwa nahitaji kupunguza ngare.
Nikauliza bei gani bila kondomu na bei gani kwa kondomu. Duh! jamani niazimeni kondomu .......tafadhali sina huku Bagamoyo. Yule binti bila kusita akaniambia kuwa hawezi kulala hapo kwangu kwani mtoto wake yuko nyumbani, kwahiyo bila kondomu 10.000 na tukitumia kondomu 5000.
Upo hapo? nikauliza swali inakuwaje mtoto aachwe nyumbani halafu yeye yuko hapo? Nikajibiwa hayanihusu, bali tufanye kazi(ku*******) kisha atimue zake. Nikatoa amri moja 'nenda kwenu kapumzike na mwanao, siwezi kulala na wewe wakati mwanao yuko mpweke hana mapenzi ya mama. Jamani akaniambia labda sina haja, nataka kumchezea tu kwa muda wake, nikafungua mlango nikamwabia hamna noma wewe nenda tu................
Kumbe yule mzee anakuwa na kigawo chake baada ya shughuli maana alinilalamikia vipi mjukuu unanikosesha kipato? Nikamwambia tafuta mwingine, huyo amezaa kwahiyo mimi na huyo ni mwiko.
Nikaletewa mwingine, huyu ndiye aliniacha hoi kwamba atalala hadi asubuhi hii ninavyoandika hapa, ila suala la kondomu au bila kondomu ni chaguo langu ila bei 10000. Dakika hiyo amekaa kitandani, na mzee ananiambia bei ndiyo hiyo kwahiyo kazi kwako.
Nikasema asante, waweza kwenda binti. Kitu nilichojifunza ni kwamba, niliuliza swali kwa binti huyo na mzee wa mapokezi ni kwanini anadhani kumekuwa na wimbi la ukahaba katika miji mbalimbali duniani? Nilijibiwa ni MAISHA TU. Sijui wewe unayesoma unaelewa nini maana watu wamegeuza miili yao kuwa biashara. Nimejiuliza sana kwanini binti aseme kuwa suala la kondomu ni uamuzi wangu ila anachohitaji ni malipo yake.
Mwenzangu yakanishinda, nikaomba niachwe kama nilivyo... nikawafuata rafiki zangu nikawaambia ipo kazi hapo ni 'cleverness without wisdom'.
Sasa mimi nasema naomba msaada wa kondomu maana usiku nilivyoupitisha, nimeletewa MAKAHABA wawili, halafu kahaba wa pili akaomba kondomu ili amsadie kahaba mwenzie kwakuwa dume lake halikuwa na kondomu.
Siku zote naamini utafiti wakati mwingine inabidi uingie mwenyewe ushuhudie, na mchakato wangu wa kitabu kile ni lazima niingie maeneo magumu yenye vishawishi adhimu. BASI jana usiku nilikuwa na rafiki zangu, na kwakuwa hawa jamaa wamekuja na Wapennzi wao, wakaanza kunishambulia eti nitajiuuuuu(ulikuwa utani) wakati tukiendelea na porojo akaja mzee wa mapokezi akaniambia 'mjukuu usipate taabu wewe sema tu sasa hivi utapata, huu ni mji wa kimataifa bwana'.
Ikabidi nitulie kisha nikamjibu hebu niletee binti mmoja nimchungulie kidogo. Wakati nipo sehemu ya chakula, chumba changu nimekifunga, kumbe yule mzee akampigia simu kahaba mmoja hivi, nadhani anafahamiana nao. Akajiingiza hapa kwenye nyumba tuliyopo, lakini mlango wangu ukawa umefungwa(sikuwepo).
Punde niliporejea, nikaona mzee ananilaumu mbona binti alikuja, ila ameahidi kuwa atakuja tena. Kweli zilipita dakika 15 hivi, nikiwa chumbani naongea na rafiki zangu, mara mlango ukagongwa na yule mzee, nikawaambia jamani waungwana nendeni chumbani kwenu. Mzee akanikabidhi binti tuelewane......
Akakaa kitini na kuniambia anisikiliza, ikabidi niulize inakuwaje mbona unanijia? Akaniambia kuwa alielezwa na mzee kuwa nahitaji kupunguza ngare.
Nikauliza bei gani bila kondomu na bei gani kwa kondomu. Duh! jamani niazimeni kondomu .......tafadhali sina huku Bagamoyo. Yule binti bila kusita akaniambia kuwa hawezi kulala hapo kwangu kwani mtoto wake yuko nyumbani, kwahiyo bila kondomu 10.000 na tukitumia kondomu 5000.
Upo hapo? nikauliza swali inakuwaje mtoto aachwe nyumbani halafu yeye yuko hapo? Nikajibiwa hayanihusu, bali tufanye kazi(ku*******) kisha atimue zake. Nikatoa amri moja 'nenda kwenu kapumzike na mwanao, siwezi kulala na wewe wakati mwanao yuko mpweke hana mapenzi ya mama. Jamani akaniambia labda sina haja, nataka kumchezea tu kwa muda wake, nikafungua mlango nikamwabia hamna noma wewe nenda tu................
Kumbe yule mzee anakuwa na kigawo chake baada ya shughuli maana alinilalamikia vipi mjukuu unanikosesha kipato? Nikamwambia tafuta mwingine, huyo amezaa kwahiyo mimi na huyo ni mwiko.
Nikaletewa mwingine, huyu ndiye aliniacha hoi kwamba atalala hadi asubuhi hii ninavyoandika hapa, ila suala la kondomu au bila kondomu ni chaguo langu ila bei 10000. Dakika hiyo amekaa kitandani, na mzee ananiambia bei ndiyo hiyo kwahiyo kazi kwako.
Nikasema asante, waweza kwenda binti. Kitu nilichojifunza ni kwamba, niliuliza swali kwa binti huyo na mzee wa mapokezi ni kwanini anadhani kumekuwa na wimbi la ukahaba katika miji mbalimbali duniani? Nilijibiwa ni MAISHA TU. Sijui wewe unayesoma unaelewa nini maana watu wamegeuza miili yao kuwa biashara. Nimejiuliza sana kwanini binti aseme kuwa suala la kondomu ni uamuzi wangu ila anachohitaji ni malipo yake.
Mwenzangu yakanishinda, nikaomba niachwe kama nilivyo... nikawafuata rafiki zangu nikawaambia ipo kazi hapo ni 'cleverness without wisdom'.
No comments:
Post a Comment