KWANINI UMEAMUA KUWA KAHABA? mmh Swali Gumu!
Ni kweli ikabidi niwe mpole, nikatuliza munkari, nikaanza kuongea kirafiki na binti huyo kwani sikuwa peke yangu bali rafiki zangu pia tumejumuika pamoja tunauliza swali hili.
Jawabu la binti huyu ni kwamba 'MAISHA', nikauliza tena je unaifurahia kwakuwa inakuingizia kipato? Nikajibiwa ni swali gumu kulijibu na nisingependa kuongelea hilo.
Nikawa na adabu, nikajaribu kudodosa tena, unajiamini vipi kukubalia kulipwa 10000 bila kutumia kondomu, na 5000 kwa kondomu? Nikajibiwa..... naomba iwe mwisho.... halafu akanitusi mse***** nini,. Ni matumaini yangu hakunilewa lakini baada hakika nakwambia akawa rafiki mwema tu licha ya kazi ya kuuza mwili wake.
Yaani ndani ya nusu saa amehudumia watu wawili wa vyumba tofauti, halafu katika trip hii kuna watu wana wake zao, na wanajivinjari kana kwamba wake zao hawawatoshi, na utadhani hii ni tour ya mwaka mzima wakati ni siku chache tu.
Suala la msingi nimejifunza sana neno 'MAISHA' kwasababu kila unayeongea naye kishkaji anakwambia MAISHA MTU WANGU. Sasa hapo najiuliza tufanye nini ili kuwaondoa watu katika ngome hiyo waliyopo? Sasa kwasababu wanalalamikia kuwa MAISHA, ni wazi hawa ni wahanga wa MAISHA ya kila siku, lakini ni MAISHA gani hayo?
Bila shaka nawe msomaji unaelewa anapokujibu MAISHA, na ikafika mahali kuna binti aliangusha kilio, tukamwomba msamaha, endapo tunamwudhi, lakini hakika nimebaini makahaba hawa kila mmoja analo DUKUDUKU lake, lakini hawajapata mahali sahihi pa kulisema suala hilo. Sijui ni DUKUDUKU gani, na labda ni MAISHA MTU WANGU.
Jamani nipo fasta nabasti kama pancha, sasa tunaenda zetu makumbusho ya watu wa kale hapa. Hii ndiyo BAGA-HEART mji mtamu nimeupenda jamani hadi raha......halafu mmoja akasema... nyie jamaa poa sana, oyaa nitakupeni namba zangu au vipi mkija tena tuwasiliane...... ha ha ha ha nikupe namba msomaji nawe upatiwe HUDUMA? Thubutu.... sikupi ng'ooooooooooooooooooooooooooooooooo, utajijuuuuuuuuuuu
No comments:
Post a Comment